Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, hafla hiyo ilijumuisha hotuba ya Hujjatul-Islam Sayyid Saeed Khalkhali, aliyezungumzia kuhusiana na mwenendo wa maisha binafsi wa Bibi Fatima (a.s.) na umuhimu wa kushiriki katika masuala ya kijamii.
Katika maelezo yake, alibainisha nafasi ya kipekee ya Bibi Fatima (a.s.) katika mfumo wa Ahlul-Bayt (a.s.) akisema: “Kumjua Fatima Zahra (a.s.) ni kumjua mwanadamu mkamilifu. Yeye hakuwa tu binti wa Mtume (s.a.w.w) na mke wa Imam Ali (a.s.), bali alikuwa taswira halisi ya imani, uchamungu, elimu, na uwajibikaji mbele ya Mwenyezi Mungu na jamii.”
Chanzo: Idara ya Mahusiano ya Umma na Habari ya Shirika la Utamaduni na Mawasiliano ya Kiislamu.
Maoni yako